Wednesday, December 13, 2017

Waziri Mkuu Majaliwa kuongoza shughuli za kuaga miili ya wanajeshi 14 waliouawa DRC



Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kasim Majaliwa,kesho Desemba 14,2017 anatarajia kuwaongoza waombolezaji kwenye shughuli ya kuaga miili ya wanajeshi 14 wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania JWTZ waliouawa wakati wakitekeleza majukumu ya kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo,DRC
Taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano Makao Makuu ya JWTZ imeeleza kuwa shughuli ya kuaga miili hiyo itafanyika katika viwanja vya makao makuu ya JWTZ yaliyopo Upanga jijini Dar es salaam
Taarifa hiyo imeeleza kuwa shughuli ya kuaga itaanza mapema asubuhi na kuhudhuriwa pia na Mkuu wa Majeshi Jenerali Venance Mabeyo na wakuu wengine wa vyombo vya ulinzi na usalama

Aidha imeongeza kuwa baada ya kukamilika kwa shughuli ya kuaga,miili hiyo itasafirishwa kwenda makwao kwa ajili ya mazishi
Wanajeshi hao 14 waliuawa baada ya kushambuliwa na waasi wakati wakitekeleza jukumu la kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo chini ya vikosi vya Umoja wa Mataifa ambapo katika shambulio hilo,wanajeshi wengine 44 walijeruhiwa na wawili wengine hawajulikani walipo


JIFUNZE NAMNA YA KUENDESHA BIASHARA YAKO HAPA KWA HUYU NDUGU.

KAMA UNA NDOTO YA  # KUJIJIRI  AU KUFANYA  # BIASHARA  USIOGOPE ILA JIFUNZE KIDOGO HAPA! Naitwa Andrea. Na nakutana na watu we...