Wednesday, April 13, 2016

YANGA: Tunawasubiri MTIBWA SUGAR

April 13 klabu ya Dar es Salaam Young Africans iliendelea na harakati zake za kumaliza viporo vya mechi za Ligi Kuu soka Tanzania bara, klabu ya Yanga ilikuwa na viporo vitatu ila April 13 2016 imemaliza mchezo wake wa pili wa kiporo dhidi ya klabu ya Mwadui FCya Shinyanga.
Yanga waliingia uwanjani wakiwa wanajua umuhimu wa mchezo dhidi ya Mwadui FC, kwani ilikuwa ni lazima wapate point tatu ili wajiweke katika nafasi nzuri, Yangawalifanikiwa kuibuka na ushindi wa goli 2-1, magoli ya Yanga yalifungwa na Simon Msuva dakika ya 4 na Haruna Niyonzima dakika ya 87, wakati Mwadui FC waliambulia goli la kufutia machozi kupitia kwa Kelvin Sabato dakika ya 14.

No comments:

Post a Comment

JIFUNZE NAMNA YA KUENDESHA BIASHARA YAKO HAPA KWA HUYU NDUGU.

KAMA UNA NDOTO YA  # KUJIJIRI  AU KUFANYA  # BIASHARA  USIOGOPE ILA JIFUNZE KIDOGO HAPA! Naitwa Andrea. Na nakutana na watu we...